Mwakilishi maalumu wa UN kwa Umoja wa Afrika, Parfait Onanga-Anyanga, amehitimisha ziara yake Tanzania ambapo amekutana na Rais Samia kujadili vurugu za uchaguzi wa Oktoba 29.
Rais Samia ameahidi kuzingatia sheria, uwajibikaji na utulivu wa nchi, pamoja na kupokea mapendekezo ya tume ya uchunguzi iliyoongezewa muda.
Onanga-Anyanga amesema atawasilisha tathmini yake kwa Katibu Mkuu wa UN na kusisitiza umuhimu wa mazungumzo jumuishi. Pia amekutana na vyama vya siasa ambavyo vimeibua masuala ya kasoro za uchaguzi, katiba, na kutokuwa na imani na tume ya uchunguzi.
Chanzo; Dw