Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Samia, Nguvu Tulioitumia Inaendana na Vurugu Zilizotokea

 Rais Samia Suluhu Hassan amesema nguvu iliyotumika na Serikali kudhibiti vurugu, iliendana na ukubwa wa tukio lenyewe na kwamba ameapa kuilinda nchi, mipaka yake na usalama wa raia wake.

Ilivyofanywa na Serikali siku hiyo, amesema ndivyo inavyofanyika katika mataifa mbalimbali kunapotokea tukio la vurugu zinazotishia usalama wa raia na Taifa kwa ujumla.

Rais Samia ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam leo, Jumanne Desemba 2, 2025 alipozungumza katika kikao chake na wazee wa jiji hilo.

“Sasa tunapoambiwa kwamba tulitumia nguvu kubwa sana kwenye tukio lile, nguvu ndogo ilikuwa ni ipi? Ilikuwa tuwaangalie waandamanaji waliojiandaa kufanya mapinduzi mpaka wafanikiwe? Hapo patakuwa pana dola kweli, dola haipo hivyo,” amesema.

Rais Samia amesema jambo kama hilo, limeshuhudiwa pia katika maeneo mengine mengi, panapotokea vurugu kama hizo, Serikali hutumia nguvu kubwa kudhibiti.

“Sasa wanapokuja kutulaumu mlitumia nguvu kubwa, wao walitaka nini,?

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: