Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Mchengerwa Aanza Utekelezaji Kutozuia Maiti Hospitalini

Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa ameagiza hospitali zote nchini kuanza mara moja utekelezaji wa katazo la kuzuia maiti kwa sababu ya madeni ya matibabu, akisisitiza kuwa agizo hilo ni la lazima na halitakiwi kukaidiwa.

Amesema hakuna Mtanzania atakayenyimwa huduma ya matibabu kwa kukosa fedha wala familia kunyimwa mwili wa mpendwa wao, akibainisha kuwa vitendo vya kuzuia maiti vinakiuka utu na maadili ya Taifa.

Mchengerwa amezitaka hospitali kutafuta vyanzo mbadala vya mapato badala ya kuwaumiza wananchi, akionya kuwa viongozi watakaokiuka agizo hilo watachukuliwa hatua za kisheria na kinidhamu.

Ametoa agizo hilo leo Desemba 8, 2025 alipokuwa akizungumza kwenye kikao kazi na watumishi wa sekta ya afya kilichofanyika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), akisisitiza kuwa utekelezaji wake utafuatiliwa kikamilifu katika hospitali zote za umma na binafsi.

“Wizara itaendelea kufanya ukaguzi wa kushtukiza kuhakikisha wananchi wanapata huduma kwa haki, staha na ulinzi wa utu wao hata baada ya kifo,”amesisitiza Mchengerwa.

 

Chanzo; Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: