Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Mv Kazi Yasimamisha Huduma, Daraja Njia Mbadala kwa Baiskeri na Vyombo vya moto

Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) umetangaza kusimamishwa kwa muda kwa huduma ya Kivuko cha MV KAZI katika eneo la Posta – Kigamboni baada ya kuibuka kwa changamoto kwenye mifumo yake ya uendeshaji.

Kupitia taarifa iliyotolewa leo, Novemba 24, 2025, TEMESA imeeleza kuwa mafundi wake wako katika kivuko hicho wakishughulikia tatizo hilo ili kurejesha huduma haraka iwezekanavyo.

“Mafundi wetu wako kwenye kivuko wakijaribu kutatua changamoto iliyojitokeza. Huduma kwa sasa inaendelea kutolewa na vivuko vya Azam Sea Taxi,” imeeleza taarifa hiyo.

Aidha, TEMESA imewataka watumiaji wa magari, pikipiki na baiskeli kutumia Daraja la Mwalimu Nyerere, kwani vivuko vinavyoendelea kutoa huduma kwa sasa vinabeba abiria pekee.

Wakala huo pia umeomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na kuahidi kutoa taarifa zaidi pindi matengenezo yatakapokamilika.

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: