Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Sababu za Mwanafunzi Aliyefariki UDOM Kujitumbukiza Kisimani

Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Said Kabuga amefariki dunia baada ya kutumbukia kwenye kisima huku taarifa zikieleza kuwa ni hofu ya kupoteza fedha nyingi kwenye kamali.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gallus Hyera amethibitisha tukio hilo akisema taarifa za awali zinaonyesha alijitupa mwenyewe kisimani.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo Jumatano Novemba 26, 2025 ambapo simu na vifaa vingine vimekutwa juu ya kisima hicho.

"Ni kweli taarifa hizo tunazo, lakini kinachoonyesha ni kwamba alijitupa kisimani mwenyewe kwa kujiandaa na bado kuna mambo tunayachunguza," amesema Kamanda Hyera.

Kwa mujibu wa wanafunzi wenzake, Kabuga alikuwa mwaka wa pili anasoma Shahada ya Uandishi wa Habari na Uhusiano wa Umma na inaelezwa hakuwa na tatizo katika maisha yote akiwa mwaka wa kwanza chuoni hapo.

"Naomba msiniandike jina langu, lakini jamaa alibeti jana fedha za ada na baadaye alianza kulalamika kuwa itakuwaje kwa wazazi wake, ile hofu hata chakula cha jioni hakula," amesema mmoja wa wanafunzi.

 

Chanzo; Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: