Wanafunzi watatu wa Shule ya Msingi Msongola, iliyopo Kivule wilayani Ilala, jijini Dar es Salaam, wamefariki dunia baada ya kupigwa na radi.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, amethibitisha tukio hilo, akieleza kuwa limetokea leo Jumatano, Machi 18, 2026.
Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo, huku wananchi wakitakiwa kuchukua tahadhari wakati wa mvua ili kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na radi.
Chanzo; Global Publishers