Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Kifo cha Hassan Chashtua Wananchi Alikuwa Akikimbia Akiomba Msaada

Kijana aliyefahamika kwa jina la Hassan Shabani (17), mkazi wa Kigamboni, Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi, amefariki dunia kwa kudaiwa kuchomwa kwa kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake.

Tukio hilo limedaiwa kufanywa na watu ambao hadi sasa hawajajulikana, ambapo mashuhuda wamesema kuwa marehemu alikuwa akikimbia huku akiomba msaada kabla ya kupoteza maisha.

Baba mzazi wa marehemu, Shabani Hasani, amesema alipokea taarifa za tukio hilo kutoka kwa mke wake akiwa shambani. Kwa upande wake, Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Kigamboni, Deogratius Mweli, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Katika hatua nyingine, wananchi wa mtaa huo wametakiwa kushikamana na vyombo vya usalama kukomesha vitendo vya uhalifu, hususan makundi ya vijana wahalifu maarufu kama “dam chafu”

 

 

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: