Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Jk Ajibiwa Maombi Yake na Dkt. Nchimbi

Rais mstaafu wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania awamu ya nne  na mkuu wa chuo kikuu cha Dar es salaam Dkt Jakaya Mrisho  Kikwete, amemuomba Makamu wa Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi  kuongezewa ardhi  ya kutosha kwenye chuo kikuu cha Dar es Salam Kampasi ya Kagera kwa mahitaji  ya sasa na siku zijazo

Chuo kikuu cha Dar es salaam kampasi ya Kagera kinajengwa katika wilaya ya Bukoba mkoani kagera kata Karabagaine chenye ukubwa wa ardhi yenye hekari zaidi ya miamoja ambazo zimetolewa bure  na wanakijiji wa Itahwa na Kangabusharo katika kata hiyo  kwa kuchangia maendeleo ya sekta ya elimu nchini

Dkt Kikwete ametoa ombi hilo baada ya uwekaji wa jiwe la msingi katika kampasi ya  chuo hicho kinachojengwa kwa  mkopo  wa mashart nafuu kutoka benki ya dunia kwa thamani ya sh bilioni 14 ikiwa ni matayarisho ya utekelezaji wa wa mradi wa elimu ya juu kwa mageuzi ya kiuchumi Tanzania

Makamu wa Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzani Mhe Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi amesema maombi hayo wanayafanyia kazi huku akiiagiza wizara ya ujenzi pamoja na  wizara ya elimu sayansi na Tecknologia kushirikiana na wadau wengine kuhakikisha taratibu na mahitaji mengine ya muhimu kuandaliwa mapema ili kuwezesha chuo kikuu cha  Dar es salam  kampasi ya  Kagera  kuanza bila vikwazo.

Mkuu wa mkoa wa Kagera Hajat Fatma Mwassa amemshukuru Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mhe  Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea chuo hicho ambacho kinachotarajiwa kufunguliwa mwanzoni mwa mwaka ujao (2026) na kitaanza kubeba wanachuo zaidi ya 800 na kufikia wanachuo zaidi ya elf moja ifikapo 2030.

 

Chanzo; Clouds Media

Kuhusiana na mada hii: