Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Mbunge Aliyebabaika Kuapa “Ripoti za Miaka 5 Sikusomewa na mtu”

Mbunge wa Jimbo la Kwahani, Zanzibar, Mkoa wa Mjini, Mohammed Abdallah Makame (Laki), leo Novemba 23 ametembelea Jimbo la Kwahani kwa mara ya kwanza tangu aapishwe kuwa mbunge wa jimbo hilo.

Laki amefanya ziara ya kuwatembelea wananchi wa jimbo hilo, huku akiwakumbusha kuhusu vipaumbele alivyowaahidi wakati akiomba ridhaa ya kuwaongoza.

Mbunge huyo ametumia nafasi hiyo kufafanua kilichotokea bungeni wakati wa kuapishwa, ambapo alionekana kubabaika na kupata kigugumizi wakati wa kuapa.

Amesema bado hajajua nini kilitokea, kwani tayari ameshawahi kuapa mara kadhaa akiwa diwani na pia amewahi kuwasilisha ripoti mbalimbali katika shughuli zake za kisiasa ndani ya chama na maeneo mengine.

 

Chanzo; Global Publishers

Kuhusiana na mada hii: