Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Lissu Ataka Kuzingatiwa Taarifa ya AU, SADC Kuhusu Uchaguzi

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu ametaka kuzingatiwa kwa maoni yaliyotolewa na waangalizi wa uchaguzi kutoka Umoja wa Afrika (AU) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuhusu uchaguzi.

Kwa mujibu wa taarifa ya chama hicho iliyomnukuu mwenyekiti wao huyo ambaye yuko gerezani Ukonga kutokana na mashtaka ya uhaini yanayomkabili, Lissu anaunga mkono taarifa zilizotolewa na waangalizi hao wa uchaguzi akisema zimeonesha uhalisia wa hali ilivyokuwa kabla, baada na wakati wa uchaguzi.

Katika taarifa ya SADC ilisema kuwa uchaguzi wa Tanzania uliofanyika Oktoba 29, kuwa haukukidhi viwango vya kidemokrasia vilivyowekwa na jumuiya hiyo taarifa ambayo iliungwa mkono na ile ya AU.

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: