Wakazi wa Kijiji cha Buzegwe wilayani Ukerewe mkoani Mwanza, wameomba Serikali kufanya uchunguzi wa kina kuhusu tukio la Mwanafunzi kukamatwa na Mamba na baada ya siku saba mwanafunzi huyo kurudishwa katika eneo aliloshambuliwa kandokando ya Ziwa Victoria akiwa hai.
Tukio hilo linadaiwa kutokea Machi 2, 2026, katika Kitongoji cha Ilondo Magharibi, Kijiji cha Buzegwe, Kata ya Kagunguli, hali hii imeibua maswali miongoni mwa wakazi wa eneo hilo na wanafamilia.
Chanzo; Itv