Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Meli za Marekani, Israel Zapigwa Marufuku Kukatiza Harmuz

Waziri wa mambo ya nje wa Iran bwana Abbas Araghachi ametangaza rasmi kwamba Mlango wa Bahari wa Hormuz (Strait of Hormuz) haujafungwa kwa dunia nzima, bali umezuiwa tu kwa Marekani, Israel na washirika wao.

Kwa mujibu wa tangazo hilo, meli za biashara kutoka nchi nyingine duniani zitaruhusiwa kupita kwa uhuru katika njia hiyo muhimu ya kimataifa ya usafirishaji wa mafuta.

Tamko hilo linaeleza kuwa madai ya Washington kwamba njia hiyo imefungwa kwa dunia yote hayana msingi, huku taarifa hiyo ikitangazwa hadharani kwenye matangazo ya moja kwa moja ya televisheni.

 

 

 

 

Chanzo; Global Publishers

Kuhusiana na mada hii: