Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Ukraine Yashambulia Meli za Urusi Bahari Nyeusi

Ndege zisizo na rubani za Ukraine zimeshambulia meli mbili za mafuta zinazojulikana kama 'shadow fleet' za Urusi zilipokuwa zikisafiri kupitia bahari nyeusi, maofisa wa Ukraine wamesema.

Picha zilizothibitishwa na BBC zinaonyesha ndege zisizo na rubani zikipita kwa kasi kwenye mawimbi hadi kwenye meli hizo, kabla ya kulipuka na kuwasha moto na kupelekea moshi mweusi kuonekana angani.

Meli za mafuta zilizolengwa zilitajwa na mamlaka ya Uturuki kama Kairos na Virat, zote zikiwa na alama ya Gambia. Zote mbili zilishambuliwa pwani ya Uturuki siku ya Ijumaa, na Virat iliripotiwa kushambuliwa tena siku ya Jumamosi. Hakuna majeruhi walioripotiwa.

Mashambulizi hayo yanaonekana kuzidishwa na Kyiv inapojaribu kuathiri mapato ya mafuta ya Urusi, ambayo ni muhimu kwa kufadhili vita vyake nchini Ukraine.

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: