Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Trump Aichomoa Canada Bodi ya Amani

Rais wa Marekani Donald Trump amefuta mwaliko wa Waziri Mkuu wa Canada Mark Carney kujiunga na Bodi yake ya Amani.

Rais Trump ametangaza katika chapisho lake kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social, bila ya kutoa sababu ya kuchukua hatua hiyo.

Awali Trump alilalama kwamba Carney ni mtu asiye na shukrani na kuongeza kuwa Canada ipo kwa sababu ya Marekani, huku akimuonya Carney kukumbuka hilo anapotoa matamshi yake.

Canada ni moja ya mataifa ambayo hayakuthibitisha kujiunga na Bodi hiyo iliyozinduliwa Alhamisi na Carney alisema kimsingi nchi yake inaweza kushiriki, lakini bado kuna masuala ambayo hayajakamilika

Trump alizindua rasmi bodi hiyo mpya jana katika Jukwaa la Uchumi Duniani huko Davos, Uswisi, ambayo wakosoaji wanaiona kama itakayokuwa mpinzani wa Umoja wa Mataifa.

 

 

 

Chanzo; Eatv

Kuhusiana na mada hii: