Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Bobi Wine Apewa Saa 48 Kujisalimisha

Katika hatua iliyoibua taswira ya wasiwasi kisiasa nchini Uganda, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini humo (CDF), Jenerali Muhoozi Kainerugaba, ambaye pia ni mtoto wa Rais Yoweri Museveni, ametangaza kupitia mtandao wa X kumsaka kiongozi wa upinzani, Bobi Wine.

Katika taarifa hiyo iliyosambaa na kuzua mjadala mitandaoni leo Jumanne Januari 20, 2026, Muhoozi amempa Bobi Wine saa 48 kuhakikisha anajisalimisha kwa polisi.

Amesema iwapo Bobi Wine hatatimiza agizo hilo, atachukuliwa kuwa ni mhalifu, atatafutwa kwa operesheni za kihalifu.

Aidha, taarifa ya kumhusu Bobi Wine imekuja katika mfululizo wa taarifa nyingi ambazo Mkuu huyo wa Majeshi ya Uganda amekuwa akiziweka kwa nyakati tofauti tangu kumalizika kwa uchaguzi huo, akitaja operesheni za jeshi hilo kwa wahalifu na hatua linazochukua.

“Ninampa saa 48 kamili kujitokeza mbele ya Polisi, asipofanya hivyo tutamchukulia kama mhalifu au mkaidi na tutamkabili ipasavyo,” amesema Muhoozi kwenye ukurasa wake wa X.

 

 

Chanzo; Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: