Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Trump Avujisha Meseji za Nyeti na Kiusalama

Rais wa Marekani Donald Trump ameibua mjadala mpana wa kimataifa baada ya kuweka hadharani ujumbe binafsi aliotumiwa na Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, kupitia mtandao wake wa kijamii wa Truth Social, hatua iliyozua maswali kuhusu maadili ya diplomasia na faragha ya mawasiliano ya viongozi wa dunia.

Katika ujumbe huo, Rais Macron anaonekana kuzungumzia masuala nyeti ya kisiasa na kiusalama, akionyesha kuwa yeye na Trump walikuwa tayari wamefikia makubaliano kuhusu mzozo wa Syria na pia mipango ya ushirikiano wa pamoja kuhusu Iran. Hata hivyo, Macron alionyesha mshangao wake kuhusu msimamo wa Marekani juu ya Greenland, akisema hakuwa anaelewa kinachoendelea katika eneo hilo.

 

 

 

Chanzo; Global Publishers

Kuhusiana na mada hii: