Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Bilioni 15 za Mauzo ya Hisa Kutumika Kutanua JKIA

Kenya imesema itatumia kiasi shilingi bilioni 15 hadi 20 sawa na dola milioni 155 za kimarekani kutoka kwenye kiwango ilichokusanya kupitia mauzo ya awali ya hisa za Kampuni ya Bomba la Mafuta ili kufanya upanuzi wa kiwanja chake cha ndege cha kimataifa kilichopo mjini Nairobi.

Hayo yameelezwa na Rais William Ruto wa nchi hiyo. Serikali ya Kenya ilitangaza wiki iliyopita kwamba imepata shilingi bilioni 106.3 kwa kuuza asilimia 65 ya hisa zake kwenye kampuni ya taifa ya Bomba la Mafuta na kwamba itatumia fedha hizo kufadhili miradi ya miundombinu ikiwemo barabara, reli na bandari.

Rais Ruto amesema upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta utakuwa mradi wa kwanza mkubwa utakaofadhiliwa chini ya mkakati huo mpya wa kutafuta fedha.

 

 

Chanzo; Dw

Kuhusiana na mada hii: