Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Marekani Yaitisha ICC Ikimchunguza Trump

Utawala wa Rais wa Marekani Donald Trump umeitaka Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita, ICC, kuachana na mipango yoyote ya kumchunguza na hata kumshtaki Rais Trump na maafisa wa utawala wake pale watakapomaliza muda wao mwaka 2029.

Utawala wa Trump umeitaka mahakama ya ICC kufanya marekebisho katika sheria yake ya msingi ili kuhakikisha haimchunguzi wala kumshtaki Rais huyo wa Marekani hapo baadaye.

Kulingana na afisa wa serikali ya Trump aliyezungumza kwa sharti la kutokutajwa jina, Utawala huo umeahidi vikwazo dhidi ya mahakama hiyo kama itashindwa pia kuachana na uchunguzi wa awali dhidi ya wanajeshi wa Marekani kutokana na vitendo vyao nchini Afghanistan na kesi dhidi ya viongozi wa Israel.

 

Chanzo; Dw

Kuhusiana na mada hii: