Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Marekani Yajiondo WHO Rasmi

Serikali ya Marekani, chini ya utawala wa Rais Trump, imetangaza rasmi kukamilisha mchakato wa kujiondoa katika Shirika la Afya Duniani (WHO) siku ya Alhamisi. Hatua hii inakuja ikiwa ni mwaka mmoja kamili tangu Rais Trump aliposaini amri ya mtendaji kuanza mchakato huo, ikiashiria mabadiliko makubwa katika uhusiano wa Kimataifa wa nchi hiyo kwenye sekta ya afya.

Afisa mwandamizi wa Idara ya Afya na Huduma za Binadamu (HHS) ameeleza kuwa uamuzi huo umetokana na madai kuwa WHO imepoteza mwelekeo wa dhamira yake ya msingi. Serikali imesisitiza kuwa katika matukio kadhaa, shirika hilo limekuwa likitenda kinyume na maslahi ya Marekani katika kulinda afya ya umma, jambo lililopelekea nchi hiyo kusitisha ushirikiano na ufadhili wake.

 

 

 

Chanzo; Itv

Kuhusiana na mada hii: