Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Cameron Kiongozi wa Upinzani Akimbilia Gambia

Kiongozi upinzani nchini Cameroon, Issa Tchiroma Bakary, amekimbilia nchini Gambia, kwa mujibu wa taarifa ya Serikali ya Gambia iliyotolewa hapo jana.

Tchiroma, aliyegombea urais katika uchaguzi wa Oktoba na ambaye anapinga matokeo yaliyomrejesha madarakani Rais Paul Biya, anadaiwa kuwasili nchini Gambia tangu Novemba 7 kwa misingi ya kibinadamu na kwa lengo la kulinda usalama wake.

Hatua hiyo inakuja wakati majadiliano ya kidiplomasia na juhudi za kusaka suluhu ya amani kuhusu mvutano wa baada ya uchaguzi nchini Cameroon yakiendelea. Tchiroma anasisitiza kuwa ndiye mshindi wa uchaguzi huo, na mara kadhaa aliwahamasisha wananchi kuandamana kupinga matokeo.

Wakati huohuo, Serikali ya Cameroon imesema itamfungulia mashtaka ya kuhamasisha maandamano, ambayo imekuwa ikisababisha usumbufu na kusimamisha shughuli mbalimbali nchini humo.

 

Chanzo; Crown Media

Kuhusiana na mada hii: