Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

M23 Yataka Waliotoroka Uvila Kurejea Nyumbani

Msemaji wa waasi wa M23, Lawrence Kanyuka, ametoa wito kwa wakazi wa mji wa kimkakati wa Uvira, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambao walikimbia kutokana na mapigano makali, kurejea katika makazi yao.

Hii inakuja baada ya M23 kuthibitisha kuuteka kikamilifu mji wa Uvira, kufuatia makabiliano makubwa kati ya wapiganaji wa kundi hilo na Jeshi la Serikali ya Kongo (FARDC), mapigano ambayo yalianza mapema mwezi huu.

Taarifa zinasema kuwa wakaazi wengi wa Uvira wamekimbilia Burundi, hasa kutokana na ukaribu wa mji huo na Bujumbura, licha ya M23 kuahidi usalama kwa wanaorejea.

Wakati huo huo, mataifa mbalimbali yakiwemo Marekani yanaendelea kusisitiza umuhimu wa utulivu na mazungumzo ya kumaliza mgogoro huo unaoendelea kutikisa eneo la Mashariki mwa Kongo.

 

Chanzo; Global Publishers

Kuhusiana na mada hii: