Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Mbappe Kuzikuta Rekodi za Messi na Ronaldo

Mshambuliaji wa Ufaransa, Kylian Mbappé, ameweka rekodi ya kipekee katika ulimwengu wa soka baada ya kuwa mchezaji wa nne duniani katika karne ya 21 kufunga magoli 60 au zaidi ndani ya mwaka mmoja kwa upande wa klabu na timu ya taifa.

Hatua hiyo inamuweka mshambuliaji huyo wa Real Madrid kwenye orodha ya wachezaji wachache sana waliowahi kufikisha idadi ya mabao 60 au zaidi, orodha ambayo awali iliwahusisha magwiji kama Lionel Messi, Cristiano Ronaldo na Robert Lewandowski.

Mbappé amefikia mafanikio hayo makubwa huku bado akiwa na mechi kadhaa zilizobaki kabla ya kufikia Januari Mosi 2026, jambo linaloongeza uwezekano wa kuifanya rekodi yake kuwa kubwa zaidi.

Lionel Messi - mabao 91 (2012)
Cristiano Ronaldo - mabao 60 (2011)
Cristiano Ronaldo - mabao 63 (2013)
Robert Lewandowski - mabao 69 (2021)

 

Chanzo; Eatv

Kuhusiana na mada hii: