Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Arteta Auvunja Ukimya Aanika Kikosi

Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta, ametoa taarifa ya wachezaji majeruhi kuelekea mechi ya Ligi Kuu England dhidi ya Wolves.

Arteta amesema beki wa Ufaransa William Saliba anakaribia kurejea uwanjani baada ya kukosekana tangu Novemba 26.

Hata hivyo kocha huyo raia wa Hispania amesema, ataangalia mazoezi ya leo ili kuthibitisha kama beki huyo atacheza katika mechi ya kesho Jumamosi, Desemba, 13, 2025.

“Kama ni mechi dhidi ya Everton wiki ijayo, naamini atakuwa fiti. Kwa kesho bado hatujui.”

Kuhusu wachezaji wengine kama Jurrien Timber, Declan Rice na Leandro Trossard, Arteta hajathibitisha kama watakuwa tayari baada ya kukosa mechi dhidi ya Club Brugge.

Mashabiki wa Arsenal wanatarajia kwa hamu kuona nani atarejea kuongeza nguvu kwenye kikosi cha Arteta katika mechi zijazo.

 

Chanzo; Mwanaspoti

Kuhusiana na mada hii: