Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Hatima ya Mo Salah Anfield

Mshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah, ameashiria kuwa huenda mchezo wa dhidi ya Brighton ukawa mechi yake ya mwisho kabisa katika uwanja wa Anfield.

Akizungumza na ViaPlay, Salah alisema:

“Niliwapigia mama na wazazi wangu nikawaambia… njoo kwenye mechi dhidi ya Brighton. Sijui kama nitacheza au la, lakini nitaifurahia kwa hali yoyote.”

Salah pia aliongeza kuwa ana mpango wa kuwapo Anfield kuwaaga mashabiki kabla ya kujiunga na Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON)

“Nitakuwa Anfield kuwaaga mashabiki… kisha niende kwenye Kombe la Afrika. Sijui nini kitatokea nikiwa huko, sijui nini kitaendelea baadaye.”

Akitamka hisia zake za kudumu kwa klabu hiyo, Salah alisema
“Nitaiipenda na kuisapoti Liverpool daima. Mimi na watoto wangu… Liverpool itakuwa milele timu yangu.”

 

Chanzo; Bongo 5

Kuhusiana na mada hii: