Mfanyabiashara maarufu wa Tanzania, Rostam Aziz amenunua hisa zote za Wakfu wa Maendeleo ya Kiuchumi wa Aga Khan, AKFED, katika shirika kubwa zaidi la habari Afrika Mashariki, Nation Media Group, NMG, na hivyo kuwa mmiliki mkuu wa shirika hilo lenye vyombo mbalimbali vya habari nchini Kenya, Tanzania na Uganda - vikiwemo Daily Nation, NTV, Mwananchi Communications na Daily Monitor.
Chanzo; Dw