Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Mizigo Iliyokwama Barabarani Oktoba 29 Ili kukabidhiwa Vibali Vyaitajika

Kufuatia vurugu zilizofanyika siku ya Uchaguzi Mkuu 2025, Oktoba 29 zilizosababisha majanga kadhaa ikiwemo kibiashara na hata kiuchumi, Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Albert Chalamila aja na suluhisho kwa wote waliopoteza mizigo iliyokuwa ikisafirishwa kutoka sehemu moja kwenda nyingine siku ile.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Novemba 7,2025 ameweka wazi utaratibu wa namna muhusika anaweza kuupata mzigo wake.

“Polisi na vyombo dola ambavyo vimekuwa barabarani siku ya tarehe 29, yapo magari yaliyobeba mizigo ya mafuta na mizigo mingne yapo magari yaliyounguzwa kichwa lakini mzigo haukuungua.

“kwenye baadhi ya magari tulitoa barabarani mizigo na kuiweka eneo maalumu, tumeweka utaratibu kwa kusaidiana na TRA, Ewura na Jeshi Polisi kwa wale wanaodhani mizigo inawahusu watakuwa na vibali vyote vinavyohusu umiliki baada ya kujilidhisha atakabidhiwa mzigo.” Albert Chalamila

 

Chanzo; Tanzania Journal

Kuhusiana na mada hii: