Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Chatgpt Yamfelisha Kim Kardashian Mtihani

Kim Kardashian amefichua kuwa alitumia ChatGPT kujisomea kwa ajili ya mitihani yake alipokuwa chuoni akisomea sheria. Kim alitoa kauli hiyo alipokuwa na mwigizaji mwenzake wa All’s Fair, Teyana Taylor, wakati wa mahojiano yao ya tarehe 3 Novemba kwenye kipindi cha Vanity Fair’s Lie Detector Test.

Kim alisema:
“Nilikuwa natumia kwa ushauri wa kisheria. Kwa mfano, nikihitaji kujua jibu la swali, nilikuwa napiga picha na kuiweka humo ndani. Lakini mara nyingi majibu yake huwa si sahihi. Imenifanya nifeli mitihani. Halafu ninakuwa na hasira, namkemea kama, ‘Umenifeli! Kwa nini umefanya hivi?’”

Hivi karibuni, kampuni ya OpenAI imetangaza kuwa ChatGPT haitaruhusiwa tena kutoa ushauri wa kisheria au kiafya.

 

Chanzo; Bongo 5

Kuhusiana na mada hii: